Tangazo

Pages

Wednesday, May 15, 2013

MSANII DIPO AJIUNGA KWENYE MASUMBWI

Kocha wa mchezo wa masumbwi Klabu ya Amana CCM ,Kondo Nassoro Kulia akimwelekeza msanii wa michezo ya kuigiza kwenye Luninga, Haruna Mussa 'dipo' Dar es salaam jana jinsi ya kutupa makonde alipokwenda kufanya mazoezi ya ngumi kwa ajili ya kujiweka sawa sawa katika kuakikisha anafanya vizuri kwenye fani yake.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Msanii wa michezo ya kuigiza kwenye Luninga, Haruna Mussa 'dipo' akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Omari Bai wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika GYM ya Amana CCM Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Kocha wa mchezo wa masumbwi Klabu ya Amana CCM ,Kondo Nassoro Kushoto akimwelekeza msanii wa michezo ya kuigiza kwenye Luninga, Haruna Mussa 'dipo' Dar es salaam jana jinsi ya kutupa makonde alipokwenda kufanya mazoezi ya ngumi kwa ajili ya kujiweka sawa sawa katika kuakikisha anafanya vizuri kwenye fani yake.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Friday, May 10, 2013

SUPER D AFYATUA DVD TATU MPYA ZA MAFUNZO YA MASUMBWI


 
 
 
Kocha huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini,Rajabu Mhamila ‘Super D’ ametoa DVD mpya 3 kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa ngumi ndani yake kukiwa na clips za mabondia  wanaofanya vizuri Tanzania kama Thomas Mashali vs Fransic Cheka na mambondia wengine mbalimbali

CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata dvd hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo

Mbali ya kupatikana katika maeneo hayo pia
 
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD
hizo ni ya Kalama Nyilawila ,Japhert Kaseba,Rashidi Matumla, Hassani Matumla,Thomas Mashali Dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na
Francis  Miyeyusho,Japhert Kaseba na Maneno Oswald, Said Mundi na King Class Mawe. 
 
 mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali 
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

 
 
 
 

DVD MPYA ZA MASUMBWI HIZI HAPA

DVID MPYA ZA MASUMBWI KWA SASA ZIPO TAYARI KWA AJIRI KUPATA BURUDANI UKIWA NYUMBANI ZAID TUWASILIANE 0713406938 AU TEMBELEA www.superdboxingcoach.blogspot.com

Tuesday, May 7, 2013

BONDIA SAID MBELWA AMGALAGAZA SAID MKONDE KWA K,O

Bondia Omari Zungu akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Haruna Sinondo wakati wa mchezo wao uliofanyika Chanika mwishoni mwa wiki iliyopita Sinondo alishinda kwa K,O raundi ya pili picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Said Mkonde kushoto akioneshana uwezo wa kurushiana makonde na Said Mbelwa wakati wa mpambano wao uliofanyika Chanika mwishoni mwa wiki iliyopita Mbelwa alishinda kwa K,o raundi ya pili picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Said Mkonde kushoto akioneshana uwezo wa kurushiana makonde na Said Mbelwa wakati wa mpambano wao uliofanyika Chanika mwishoni mwa wiki iliyopita Mbelwa alishinda kwa K,o raundi ya pil picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Chilambo Hemed kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Boniface Urasa wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki Chanika Chilambo alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Said Mbelwa akipambana
Bondia Omari Zungu akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Haruna Sinondo wakati wa mchezo wao uliofanyika Chanika mwishoni mwa wiki iliyopita Sinondo alishinda kwa K,O raundi ya pili picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Refarii Saidi Chaku akimwinua mkono juu Bondia saidi Mbelwa kuashilia ni mshindi katika mpambano huo

Monday, May 6, 2013

MAYWEATHER Jr AMCHAPA ROBERT GUERRERO KWA POINTI

 Bondia Floyd Mayweather Jr (kushoto) akimsulubu Robert Guerrero katika pambano la masumbwi kwenye Ukumbi wa MGM Grand Garden, jijini Las Vegas, Marekani. Mayweather Jr alishinda kwa pointi pambano hilo la kwanza tangu amalize kifungo cha miezi miwili jela.
 Mayweather Jr akiendelea kumuadabisha Guerrero, kiasi cha majaji wote watatu kumpa ushindi sawasawa wa pointi 117-111 na kutwaa ubingwa wa Dunia wa WBC uzani wa ‘welter.’ 
 Guerrero akiwa na jeraha juu ya jicho la kushoto lililotokana na makonde mazito ya Mayweather Jr.
 Guerrero akipewa maelekezo na kocha wake, wakati wa mapumziko ya moja ya raundi za pambano hilo, ambalo alipigwa kwa pointi na kukiri mpinzani wake ni mjanja na ana kasi kubwa ulingoni.
 Mayweather Jr (kushoto), akikwepa fataki la kushoto kutoka kwa Guerrero katika pambano hilo.
 Guerrero akiendelea kushambulia 'upepo' kutokana na Mayweather Jr kuwa mbunifu katika kukwepa makonde yake kama anavyoonekana pichani.
 Mayweather akaweka mzaha kando na kuanza kujibu mapigo, ambapo makombora yake yalikuwa yakitua sawasawa mwilini mwa Guerrero, ingawa hayakuweza kumdondosha na kuishia kumuumiza tu na kutokwa damu.
 Guerrero akipokea konde zito la Mayweather. Baada ya pambano, Guerrero alikiri kushindwa na kumsifia mpinzani wake: "Nilimpiga baadhi ya makonde mazuri. Lakini yeye ni bondia mkubwa na bora. Ni mjanja na mwepesi mno ulingoni"
 Mayweather Jr akiwa amebebwa baada ya kutangazwa mshindi kwa pointi 177-111 kutoka kwa majaji watatu wa mtanange huo ndani ya Ukumbi wa MGM Grand Garden, Las Vegas, Marekani.
 Mayweather Jr (kulia mwenye kapero) akishangilia ushindi wake na baba yake Mayweather Sr (kushoto), huku wapambe wake wakinyanyua juu mikanda anayoishikilia baada ya ushindi wake dhidi ya Guerrero.


Mayweather baada ya pambano hilo alisema: "Najisikia vibaya kwa sababu sikuweza kushinda kwa ‘knockout’ ambayo mashabiki wangu walikuwa wakitaka. Nilipigana kadri niwezavyo kuhakikisha nashinda kwa ‘knockout,’ lakini hilo halikutokea ulingoni"

Sunday, May 5, 2013

Floyd Mayweather Jr akata ngebe za Robert “The Ghost” Guerrero

Bondia Floyd Mayweather Jr kushoto akimrushia ngumi mfululizo Robert “The Ghost” Guerrero wakati wa mpambano wao uliofanyika alfajiri ya leo
Bondia Robert “The Ghost” Guerreroakiwa chini baada ya kupata konde zito kutoka kwa Floyd Mayweather Jr  wakati wa mbambano wao uliofanyika alfajiri ya leo maywether alishinda mpambano uho kwa point
Bondia Floyd Mayweather Jr kushotoakioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Robert “The Ghost” Guerrero wakati wa mpambano wao maywether alishinda kwa point